12/02/2026
ZAMANI TUKIWA WADOGO NILIKUWA NASIKILIZA NYIMBO ZA KWAYA MBALIMBALI, MOJA YA KWAYA NILIYOSIKILIZA SANA NI KINONDONI REVIVAL KWAYA, WIMBO WANGU PENDWA ULIKUWA ULE ‘MTU WA NNE’.
•Siku moja kanisani kwetu tuliambiwa ATAKUJA MHUBIRI MGENI kutuhudumia, tukaambiwa ni MMOJAWAPO WA WAIMBAJI WA KWAYA YA KINONDONI REVIVAL, nikafurahi nikahitaji kumwona uso kwa uso mwimbaji wa kwaya ninayoipenda sana.
•Kweli, alikuja Mtumishi wa Mungu Maikos Mbwete, akatuhudumia KWA NENO LA BWANA. Alihubiri ujumbe ambao sitausahau, kichwa cha ujumbe kilikuwa “ROHO YA UWEZA”, Kutoka kwenye kitabu cha Isaya 11:2.
•Miaka mingi baadaye, nimeshakua mtu mzima; ninaandika jumbe mbalimbali huku mitandaoni, Mtumishi wa Mungu Maikos alinitafuta, akajitambulisha kwa jina nikamwambia NAKUKUMBUKA, ULIKUJA KANISANI KWETU KUTUHUDUMIA KWA NENO LA MUNGU.
Kutokea pale tukawa tunawasiliana mara kadhaa.
Jambo ambalo nilikuwa silijui kuhusu maisha yake, ni kwamba YEYE NA MKE WAKE HAWAKUWAHI KUPATA MTOTO.
-MWAKA HUU NI MWAKA WA 21, TANGU WAOANE MWAKA 2004 WALIKUWA HAWAJAPATA UZAO,
LAKINI MUNGU AMEWAKUMBUKA KWENYE MAJIRA YAKE, MWAKA HUU AMEWAPA MAPACHA!.
•MUNGU AMEIFUTA AIBU YAO, AMEONDOA HUZUNI YAO, AMEWASHANGAZA KWA KUAMUA KUFUTA MATUSI NA KEJELI.. AMEWAPA WATOTO WAWILI KWA PAMOJA.
•NILIPOONA USHUHUDA WAO, KWANZA NILISHANGAA KISHA MOYO WANGU UKAJAA FURAHA NA SHUKURANI KWA MUNGU!.
•NIMETIWA MOYO KWAMBA, HATA MAMBO UNAYOONA YAMECHELEWA MUNGU ANAWEZA AKAYAKAMILISHA KWA WAKATI WAKE.
•HAWA WATUMISHI WA MUNGU WANASHUHUDIA WANASEMA, KWA MIAKA YOTE HIYO PAMOJA NA KUTUKANWA, KUSEMWA NA KUDHIHAKIWA SANA HAWAKUWAHI KUWAZA KUMWACHA YESU, KWENDA KWA WAGANGA WALA KUCHEPUKA.. WALIENDELEA KUMWAMINI YESU NA KUIWEKA IMANI YAO KWA MUNGU!.
•MIAKA 21 NI UMRI WA KIJANA MTU MZIMA AMBAYE ANGEWEZA KUWA CHUO KIKUU SASA.. LAKINI WALIVUMILIA.
•NINACHOWEZA KUKWAMBIA KATIKA YALE UNAONA MUNGU AMEKAWIA KWAKO, USIMWACHE YESU, USIONDOE IMANI YAKO KWA MUNGU. ATAKUKUMBUKA, ATAFANYA!.
HONGERENI SANA Mr. & Mrs. Maikos Mbwete. YESU AENDELEE KUTUKUZWA KUPITIA NINYI.
Jina la Yesu LITUKUZWE!.
Shalom
_Mwl. Nick_
0712265856
(WhatsApp #)