Makutano Tv

Makutano Tv To educate, inform, entertain and inspire community through the power of online content.

WATOTO WA TANZANIA  WANAMICHEZO WAPO IRINGA TANZANIA WAKITHIBITISHA VIPAJI VILIVYOTUKUKA WAMEANZA SAFARI KUSAKA UBINGWA ...
10/06/2026

WATOTO WA TANZANIA WANAMICHEZO WAPO IRINGA TANZANIA WAKITHIBITISHA VIPAJI VILIVYOTUKUKA WAMEANZA SAFARI KUSAKA UBINGWA UMITASHUMTA 2026.

Mkakati madhubuti wa Tanzania katika kuandaa vipaji kupitia Umoja wa Michezo na Taaluma Tanzania kwa Shule za Msingi (UMITASHUMTA) 2026 unaendelea mkoani hapa Iringa.

Mashindano hayo yanayowakutanisha wanamichezo kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara pamoja na Zanzibar, ikiwemo Unguja na Pemba, yamefunguliwa rasmi Juni 9, 2026 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe.

UMITASHUMTA na UMISSETA 2026 yanaandaliwa na kuratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo.

Mashindano hayo yanafanyika chini ya kaulimbiu isemayo:

“Michezo na Sanaa Shuleni: Daraja la Ajira, Afya na Ushindani wa Kimataifa.”




2026

MAPOGORO  "B" SHULE YA MSINGI WILAYA YA  MBARALI , MBEYA.Makabidhiano ya Mradi wenye mafanikio  ( SWASH) katika  Shule y...
08/06/2026

MAPOGORO "B" SHULE YA MSINGI WILAYA YA MBARALI , MBEYA.

Makabidhiano ya Mradi wenye mafanikio ( SWASH) katika Shule ya Msingi Mapogoro B Mbarali.

Mradi huu uliotekelezwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Afya Plus kwa msaada wa Nawiri Foundation katika kuboresha miundombinu ya maliwato, chumba cha kujihafadhia kwa wasichana ( kuzingatia hedhi salama) matanki ya kuhifadhia maji safi na salama lita 10, 000 pamoja na program saidizi ili kuwezesha uelewa na ujuzi wa maarifa mapya katika mabadiliko ya tabia kwa wanafunzi.




@santation@hygiene@mbaralidistric

IRINGA YACHANGAMKA: WANAMICHEZO WA UMITASHUMTA 2026.Source: OWM-TAMISEMI,IringaWashiriki wa Mashindano ya Umoja wa Miche...
07/06/2026

IRINGA YACHANGAMKA: WANAMICHEZO WA UMITASHUMTA 2026.

Source: OWM-TAMISEMI,Iringa

Washiriki wa Mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma Tanzania kwa Shule za Msingi (UMITASHUMTA) 2026 kutoka mikoa mbalimbali nchini wameanza kuwasili mkoani Iringa kwa ajili ya kushiriki mashindano hayo ya kitaifa yanayotarajiwa kuibua na kukuza vipaji vya michezo kwa watoto wa shule za msingi.

Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Uratibu wa Michezo, Utamaduni na Sanaa katika Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Ndg. Yusuph Singo, amesema maandalizi ya mashindano hayo yamekamilika kwa kiwango cha kuridhisha na kwamba washiriki wanaendelea kuwasili na kupokelewa katika vituo vilivyotengwa.

“Washiriki wanaendelea kufika na kupokelewa kwa ajili ya hatua zinazofuata ili waweze kushiriki mashindano haya ambayo ni msingi muhimu wa kuibua na kuendeleza wanamichezo wa baadaye,” amesema Singo.

Kwa upande wake, Mratibu wa Michezo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Ndg. George Mbijima, amesema maandalizi ya miundombinu na maeneo yote yatakayotumika kwa mashindano hayo yamekamilika kwa zaidi ya asilimia 90.

“Tupo katika hatua za mwisho za maandalizi. Viwanja vimeboreshwa, waamuzi, walimu na waratibu wa michezo mbalimbali wamewasili tayari kwa kuanza kazi. Tunaamini mashindano ya mwaka huu yatakuwa bora zaidi kuliko mwaka uliopita,” amesema Mbijima.

Naye Mratibu wa UMITASHUMTA Mkoa wa Mwanza, Joseph Mambo, amesema mkoa huo ambao uliibuka bingwa wa jumla mwaka 2025 umejipanga kikamilifu kutetea ubingwa wake katika mashindano ya mwaka huu.

Mashindano hayo yanayowakutanisha wanamichezo kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara pamoja na Zanzibar, ikiwemo Unguja na Pemba, yanatarajiwa kufunguliwa rasmi Juni 9, 2026 na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe.

UMITASHUMTA na UMISSETA 2026 yanaandaliwa na kuratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo.

Mashindano hayo yanafanyika chini ya kaulimbiu isemayo:

“Michezo na Sanaa Shuleni: Daraja la Ajira, Afya na Ushindani wa Kimataifa.”

04/06/2026

Wadau wa Shirika lisilo la kiserikali ka IBO iTALIA wametoa Rai kwa jamii na Serikali kuunga mkono vipaji vya watoto wwnye mahitaji maalum

Stanley Mtweve  MWALIMU MAHITAJI MAALUM  kutola Shirika la IBO ITALIA akisheherekea mafanikio ya mchango wa IBO katika e...
30/05/2026

Stanley Mtweve MWALIMU MAHITAJI MAALUM kutola Shirika la IBO ITALIA akisheherekea mafanikio ya mchango wa IBO katika elimu na michezo Jumuishi.
Hii ni baada ya mwanafunzi asiyeona Exaud kutoka Shule ya Msimgi Kipera kushinda tuzo za BMT 2026


Jeshi la Polisi kitengo cha Dawati la Jinsia na Watoto  Iringa  kwa kushirikiana na wadau wakiwemo viongozi wa dini,  le...
21/05/2026

Jeshi la Polisi kitengo cha Dawati la Jinsia na Watoto Iringa kwa kushirikiana na wadau wakiwemo viongozi wa dini, leo wametoa elimu ya kujitambua na motisha kwa wanafunzi wasichana wanaosoma Shule ya Sekondari Mlamke iliyopo Manispaa ya Iringa.

Katika elimu ya hamasa kwa wasichana Inspekta Lidya Sospeter kutoka Dawati amehimiza wasichana kutambua mbinu sahihi za kukabili mabadiliko hasi ya kimwili yanayokinzana na tabia na maadili mema.

" nawapa mbinu bora ambayo inaweza kuwasaidia kukabili vichocheo vya mabadiliko ya mwili ni pamoja na kufanya mazoezi, kupanga ratiba na kuisimamia kwa ustadi" anasema Insp. Lidya

Aidha amewaasa mabinti kujidhatiti katika ufaulu wa masomo yao na kuwahakikishia kufikia ndoto zao iwapo watakuwa tayari kuwa mfano wa mabadiliko katika maadili mema na kuongeza kuwa kupitia Dawati la Jinsia Jeshi la Polisi limesogeza huduma rafiki kwa vijana hadi ngazi ya Kata ili kuweza kuwapatia msaada wa ushauri na kupokea taarifa katika changamoto wanazozipitia.

Pamoja naye Inspekta Lydia aliambatana na Polisi Kata ya Ilala/Makorongoni A/Insp Magreth Laizer na Afisa Ustawi
wa Kata



JUMAPILI NJEMAIRINGAWatoto KKKT Mtwivila wamejitokeza kusaidia kazi ya usogezaji tofali ktk ujenzi wa Kanisa jipya.Je ha...
17/05/2026

JUMAPILI NJEMA

IRINGA

Watoto KKKT Mtwivila wamejitokeza kusaidia kazi ya usogezaji tofali ktk ujenzi wa Kanisa jipya.

Je hapo ulipo watoto wanashiriki vipi katika shughuli za kijamii? Je wanazo taarifa za maendeleo katika Kijiji/Kata/Mtaa?

TUPE MAONI YAKO

-MMMAM

USTAWI WA JAMII WANOLEWA MALEZI PROJECTChini ya uratibu wa Mtandao wa Malezi  na Maendeleo ya awali ya Mtoto Tanzania ( ...
13/05/2026

USTAWI WA JAMII WANOLEWA MALEZI PROJECT

Chini ya uratibu wa Mtandao wa Malezi na Maendeleo ya awali ya Mtoto Tanzania ( TECDEN) Ofisi ya Ustawi Mkoa wa Iringa kwa kushirikiana na Shirika la IDYDC limewanoa maafisa ustawi manispaa ya Iringa ujio wa mradi wa vituo vya malezi mchana unaolenga kuhamasisha jamii kushiriki kikamilifu katika kuboresha vituo vya kijamii vya malezi mchana katika maeneo yao.

Mratibu wa mradi wa Mtoto Kwanza na PJTMMMAM kutoka Shirika la IDYDC REUBEN MAGAYANE
amesema Vituo vya malezi ya kijamii mchana ni huduma zinazowawezesha watoto wadogo (miaka 0-5) kupata malezi bora, lishe, na elimu ya awali wakati wazazi wakiwa kazini au kwenye shughuli za kiuchumi, zikilenga kurahisisha malezi na kupunguza mzigo kwa wazazi, hasa wanawake.

Mratibu wa Program Mkoa wa Iringa Martine Chuwa amesema kuna vituo vya kulelea watoto vya nyumbani (home-based) na vituo rasmi vya mchana (daycare centres) ambapo vituo hivyo huanzishwa kulingana na hitaji la wananchi wa eneo husika.

Aidha Chuwa ameongeza kuwa usajili na uendeshaji wa vituo hivi unasimamiwa na Kanuni za Vituo vya Kulea Watoto Wadogo Mchana za 2014 Faida za Vituo hivi vya Kijamii ni pamoja na Wanawake hupata muda wa kufanya kazi za kiuchumi. Watoto hujifunza stadi za maisha na kupata ulinzi na usalama, Kutoa huduma karibu na maeneo ya kazi.

Hata hivyo Serikali kupitia Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) imeanzisha vituo vya kijamii, ikiwa ni pamoja na vituo vilivyopo maeneo ya sokoni, kwa mujibu wa taarifa za TAMISEMI na Wizara.

Mama"s Day runners 2026
12/05/2026

Mama"s Day runners 2026

Address

Iringa
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Makutano Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share