30/06/2019
UTEKELEZAJI MATUMIZI BANDARI KAVU KWALA WAANZA!
Utekelezaji wa agizo la Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Isack Kamwelwe la kuwataka TPA na Wadau wote kuanza mara moja kutumia Bandari Kavu ya Kwala iliyopo Ruvu Mkoa wa Pwani umeanza kwa Wadau kugawana majukumu ya utekelezaji.
Hivi karibuni Waziri Kamwelwe aliunda Kamati maalumu ambayo ameipa jukumu la kuhakikisha Wadau wote wa Bandari ya Dar Es Salaam wanashirikiana na kuanza kutumia Bandari Kavu ya Kwala kufikia mwezi Julai.
Wadau hao wamekutana Julai 29 na kufanya kikao katika eneo la ujenzi wa mradi ambapo wamegawana majukumu ya kuhakikisha kila Mdau anawezesha eneo la mradi ili huduma zianze kutolewa.
Bandari hiyo ya Kwala inatarajiwa kuanza kuhudumia mzigo wa Kontena zinazosafirishwa kupitia Bandari ya Dar Es Salaam ambapo zikifika katika bandari hiyo zitasafirishwa kwa njia ya deli mpaka katika bandari hiyo na baadae kwenda katika mataifa mbalimbali.
Baadhi ya Wadau ambao wamekutana na kupatiwa maagizo ya kuanza utekelezaji ni pamoja na TPA yenyewe, Tanesco, TASAC, TAFAA, TASAA, TANROAD, Suma JKT, TRA, TATOA, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Pwani, Mamlaka ya Maji, Vyombo vya Ulinzi vya Serikali.
Katika picha ni matukio mbalimbali kuhusiana na Kikao cha Kamati hiyo.