Junior Dr

Junior Dr Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Junior Dr, upanga area, Dar es Salam.

16/05/2017

UNACHOTAKIWA KUJUA KUHUSU UGONJWA WA KISUKARI.(part 1)
Kisukari ni ugonjwa mmoja wapo kati ya magonjwa yasiyo ya kuambukizwa.ugonjwa huu humfanya mtu kuwa na kiwango kikubwa cha sukari yaani glucose kwenye damu.
Ugonjwa huu huibuka mwilini kutokana na hitilafu mbili zinazoweza kujitokeza mwilini k**a ifutavyo'
1.kongosho kushindwa kuzalisha hormone inayo itwa insulini ambayo kazi yake kubwa ni kusaidia chembechembe ndogo za mwili(cell) kutumia chakula/sukari iliyopo kwenye damu kwa ajili ya shughuli mbalimbali za mwili.upungufu wa hormone hii husababisha sukari irundamane kwenye damu.hali hii kitaalam huitwa insulin deficiency.
2.chembechembe za mwili kupoteza uwezo wa kutumia chakula/sukari iliyo katika damu kwa ajili ya shughuli za mwili na kufanya sukari ibakie nyingi kwenye damu ili hali kongosho linafanya kazi yake vizuri.hali hii kitaalamu huitwa insulini resistance.

Dalili za ugonjwa wa kisukari'
1.kujisikia kiu sana kuliko kawaida yako hali ambayo hupelekea kunywa maji mara kwa mara isivyo kawaida
2.kujisikia njaa mara kwa mara,hamu ya kula kuongezeka na kusababisha mtu kula kula muda mwingi
3.kukojoa mara kwa mara hasa wakati wa usiku

Athari za ugonjwa wa kisukari'
Ugonjwa huu ukikaa muda mrefu bila kushusha kiwango cha sukari mwilini huleta athari kubwa sana ikiwemo'
1.magonjwa ya moyo(cardiovascular diseases)
2.magonjwa ya figo(diabetic nephropathy)
3.kiharusi(stroke)
4.upofu wa macho(diabetic retinopathy)
5.vidonda visivyo pona ambavyo hupelekea mtu kukatwa viungo hasa miguu(diabetic foot)

27/01/2017

TABIA KUMI ZA ULAJI ZITAKAZO KUFANYA UISHI MAISHA MAREFU NA YENYE AFYA KEDEKEDE
1.kula asilimia 95 ya chakula unachohitaji kutoka kwenye mimea hasa mbogamboga na matunda na asilimia 5 tu kutokana na wanyama
2.kula nyama angalau mara mbili kwa week,usizidishe wala kupunguza
3.kula samaki kwa wingi uwezavyo angalau mara moja kila siku
4.furahia kula mayai angalau matatu kwa week
5.furahia kula mahage yaliyopikwa angalau nusu kikombe cha chai kila siku
6.punguza kula vyakula vyenye sukari nyingi,ukiweza tumia asali badala ya sukari ya kawaida
7.kula angalau viganja viwili vya karanga kila siku
8.kunywa maji ya kutosha kila siku hata k**a huna kiu angalau glass nane tu
9.unapo kunywa pombe tumia red wine kwa kiasi tu maana hii itakukinga na maradhi ya moyo
10.pendelea kula nafaka ambazo hazijakobolewa k**a dona kwani hizi zitakukinga na maradhi k**a cancer ya puru yaani colorectal cancer

29/12/2016

Vyakula vinavyo ongeza akili yaani(I.Q)
1. Samaki
Zaidi ya nusu ya ubongo imeundwa kwa mafuta(lipids) aina ya omega ambazo hupatikana kwenye baadhi ya samaki mfano dagaa,lipids hizi husaidia cell za ubongo kuzaliana kwa wingi na pia husaidia mfumo wa fahamu kufanya kazi vizuri na kwa ufanisi mkubwa.pia samaki wana virutubisho vingine k**a phosphorus na iodine ambavyo ni muhimu kwa kazi ya ubongo.
Kula dagaa angalau mara mbili kwa week ili uongeze I.Q yako.dagaa sio chakula cha maskini k**a wengi tunavyo dhani.

2.maziwa pamoja na mazao yake k**a samli na mtindi
Maziwa pia yana fati aina ya omega,calcium,vitamin D na magnesium.hizi huufanya ubongo uwe active muda wote na kukumbuka kwa haraka.
Kunywa maziwa angalau mara tatu kwa week,usijinyime mtindi,Horgan nk
3.main
Main yana madini ya chuma kwa wingi sana.madini haya husafirisha hewa safi ya oxygen kwa njia ya haemoglobin.ubongo unahitaji kiasi kikubwa cha oxygen ili ufanye kazi vizuri.main pia ya vitamin b1,b6,b9 na b12 ambazo ni muhimu sana kwa ustawi wa mishipa ya fahamu.
Hivo k**a kipato kina ruhusu usijinyime maini,wewe na familia yako ili muwe na IQ ya juu.
4.Mayai
Mayai yana virutubisho aina ya phospholipid na lecithin kwa wingi ambavyo ni muhimu kwa muundo na kazi ya mishipa ya fahamu
5.ndizi
Ndizi nazo zina vitamini b6 kwa wingi ambayo tumeona jinsi inavo saidia kuongeza akili

Vyakula vingine vinavyo ongeza IQ ni pamoja na parachichi na pweza na spinach

Unaweza kufanya k**a dozi kwa wanao au wewe mwenyewe .
Jaribu leo inalipaaaaaaaaaaaaaaaaaas!

04/10/2016

Mambo ya kuyajua kuhusu UTI
Huu ni ugonjwa wa njia ya mkojo unao athiri sana kibofu na figo
Ugonjwa huu husababishwa na bacteria ambao huishi kwenye njia ya chakula.hawa bacteria ni rafiki wa binadamu kwani humsaidia kumeng'enya chakula kwenye utumbo mdogo na mkubwa.
Urafiki wa hawa bacteria huisha pale tu wanapo ingia sehemu ambayo sio yake k**a vile kwenye njia ya mkojo.
Pindi wanapo ingia kwenye njia ya mkojo bacteria hawa huanza kutengeneza makazi mapya na kuharibu mirija ya mkojo,kibofu na hata figo.kwa kuwa hawa bacteria huzaliana kwa kasi kubwa yaani mara 180 kwa saa,mtu aliye pata maambikizi ya ugonjwa huu anaweza kuwa na dalili mojawapo kati ya hizi:
1.maumivu wakati wa kukojoa au kujisikia k**a mkojo unaunguza(hasa kwa wanaume)
2.maumivu ya tumbo chini ya kitovu(hasa kwa wanawake)
3.kujisikia kukojoa mara kwa mara lakini ukienda mkojo unatoka Kidogo halafu unasikilizia maumivu
4.mtoto kuchemka au kulia wakati wa kukojoa au kulia lia bila sababu
5.kukojoa mkojo wenye rangi ya mawingu mawingu

UTI HUATHIRI SANA WATOTO WADOGO NA WANAWAKE LAKINI WAMAMA WAJAWAZITO WAPO KATIKA HATARI KUBWA ZAIDI YA KUPATA UGONJWA HUU

MATIBABU:
Njia kubwa na salama ya kutibu ugonjwa huu ni kuzuia usiambukizwe,lakini ikitokea tayari umeupata kuna matibabu ya vidonge au sindano kutokana na ukubwa wa tatizo
MUHIMU:
UTI huweza kuleta matatizo ya figo k**a haukutibiwa vizuri na kwa wakati muafaka
Pia bacteria hawa wana tabia ya kuizoea dawa na kuifanya isiweze kuwaua,hivyo basi k**a wewe umekuwa ukipata maambukizi ya UTI mara kwa mara usifurahi kutumia dawa kila wakati kwani ni hatari kwa figo zako. Hivyo basi unahitaji ushauri wa kitaalam namna gani ya kuepuka ugonjwa huu.
Inalipa!!!! Itakupunguzia gharama za matibabu mara kwa mara na pia mtaji wako utakuwa salama maana afya ni mtajiiiiiiiiiii.

Address

Upanga Area
Dar Es Salam
22239

Opening Hours

Monday 06:00 - 21:00
18:00 - 19:00
Tuesday 06:00 - 21:00
18:00 - 19:00
Wednesday 06:00 - 21:00
18:00 - 19:00
Thursday 06:00 - 21:00
18:00 - 19:00
Friday 06:00 - 21:00
18:00 - 19:00
Saturday 06:00 - 21:00
18:00 - 19:00
Sunday 06:00 - 21:00
18:00 - 19:00

Telephone

0752118614

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Junior Dr posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share