Jjifunze ZaidiI

Jjifunze ZaidiI Kamara Kusupa ni Mwinjilisti anayehubiri Injili kwa viumbe wote sawa na Agizo la Yesu. Kitaaluma yeye ni mtaalamu wa sayansi ya Jamii na pia ni mtafiti wa

20/09/2021

DOI ABEL
Nimeisoma post yako ambayo imezua maswali mengi na mashaka mengi kwa Watanzania makini.
Lakini unachoshindwa kutambua ni kwamba Tundu Lissu na Mange Kimambi na Kigogo 2014 wote walimjua muuaji wa Magufuli, pia walijua jinsi alivyomuua, ndio maana wakawa wanatangaza kwa uhakika tangu kuugua kwake, kulazwa kwake hadi kufariki kwake Magufuli. SASA matukio ya Mange Kimambi aliyoyaonyesha huko New York baada ya kuwasili kwa Rais Samia yanatoa mwanga mzuri unaoonyesha kwamba hao “The Anti – Magufuli” walikuwa wakifanya kazi na watu waliokuwa ndani ya serikali ya Magufuli. Subirini mtaona zaidi kwani Mwenyezi Mungu huwa hamfichi mnafiki.

04/03/2021

HAWA NDIO WANAOUAWA NA CORONA ILA HABARI ZAO ZINAFICHWA
Nakujibu wewe Godless Lema nikiamini jibu langu litakufikia huko Canada uliko, kwakuwa unajitambulisha na waliookoka basi nakukumbusha neno la Mungu alilosema kupitia kwa Paulo Mtume wetu sisi mataifa “maana neema ya Mungu imefunuliwa nayo inawafundisha wanadamu kukataa ubaya uzidio.”
SASA ole wenu ninyi ambao hamkujifunza kumkatalia mzungu, hamjui kumwambia hapana. Mnaishi k**a kwamba Mungu aliwaleta duniani ili kumtegemea mzungu, ole wenu mnaotaka hata Watanzania wengine wakubaliane na “ukengeufu” wenu kwamba hawataishi kwa mkate tu, bali wataishi kwa kutii kila neno litokalo kinywani mwa mzungu.
OLE wako Godbless Lema uliyesahau agizo la Paulo kwamba “miongoni mwenu asiwepo mwasherati wala asiyemcha Mungu k**a Essau aliyekubali kuuza haki yake ya uzaliwa wa kwanza kwaajili ya chakula kimoja, maana mwajua hata alipoita tena baraka, hakuipata kwakuwa hakuona nafasi ya kutubu japokuwa alilia kwa uchungu”
WEWE Godbless Lema na wenzako mmeshindwa kuisimamia imani ya Yesu japokuwa mwajitambulisha na madhehebu ya kikristo, hadi leo CHADEMA yenu haijaweka msimamo ulio wazi kuhusu ndoa za jinsia moja. Mnahofia kuukorofisha Umoja wa Ulaya na wafadhili wanaowapa fedha za bure.
Mtu akiwabana wewe Godbless Lema, Tundu Lissu na Freeman Mbowe awatake mtoe tafsiri ya “homesexuality” na “Lesbisian” katika lugha ya Kichaga, Kinyaturu, Kitaturu ama Kinyiramba, mtatamka maneno gani? Maana katika kabila zote za Waafrika hakuna msamiati wa hayo, hiyvo ninyi mmeshindwa kuutetea ukristo wenu, pia mmeshindwa kuutetea hata “uafrika” wenu!
SABABU ni moja kwamba tangu muwajue wazungu hamkufundishwa kuwaambia hapana! Mwaweza kumtukana Rais wa nchi yenu, mwaweza kuwatukana hata wazazi wenu waliowazaa, lakini hamwezi kumwambia mzungu “no”!
K**a mnaweza, wakumbusheni Watanzania ni lini kwa mara ya mwisho mlipokuwa na ujasiri wa kumkatalia mzungu mkamwambia hilo kwetu ni “hapana” halitawezekana kwasababu halitekelezeki?
WATU mliokosa misimamo kiasi hicho mnaota kushika madaraka ya dola! Hivi mnawaonaje Watanzania? Mwadhani Tanzania inajiendesha peke yake? Siku zote mkae mkijua fika yuko Mungu aliye juu ya wazungu, huyo anao uamuzi wa mwisho. Hata ikitokea Watanzania kudanganyika, wakapiga kura za chuki, wakawapeni ninyi ushindi kwenye uchaguzi mkuu, bado Mungu anaweza kubadilisha matokeo kwenye dakika za majeruhi, k**a alivyobadilisha matokeo na kumrithisha Yakobo “mbaraka” wake, akamkosesha mwasherati Essau. Mwenyezi Mungu aliapa kwa hasira akisema “nimempenda Yakobo ila Essau nimemchukia, haki yake nimeirarua na kuwatupia hayawani wa mwituni” kwahiyo jiangalieni sana, Tanzania haitatawaliwa tena na waasherati wa kiroho na kiakili.
Turejee ulichoandika na ku – post mtandaoni hueleweki, masuala uliyopigia kelele tangu ukiwa Bungeni ukiwakilishi wa wananchi wa Arusha mjini hayana tija, ulitabiri kwamba Magufuli angekufa. Niliandika makala isemayo “ndugu yangu jihadhari na Roho ya ukengeufu” muda ulifika wala Rais Magufuli hakufa k**a ulivyotabiri.
Baadaye ukiwa Bungeni ulitamka kwa kinywa chako ukimwambia Spika na wote waliokusikiliza kwamba “tutakapoanza kufa (ukimaanisha sis Watanzania) wenzetu atatatucheka” wakati huo nchi jirani za Kenya, Uganda na Rwanda ziliwatangazia wananchi wao “lockdown” ambayo Magufuli aliikataa kijumla.
Kabla hujaropoka kwamba Watanzania tutakapoanza kufa wenzetu watatucheka, mke wa tajiri wa Marekani Bi Melinda Anny Gates alikuwa ametoa mapema kauli iliyofanana na ubashiri wako, alisema ifikapo Aprili 2020 Watanzania tungekuwa tunaokota maiti za watu barabarani. Huyo mke wa Bilionea Bill Gates hakutamka hayo k**a mlevi wa bangi, bali aliyasema hayo kutokana na mipango yao waliyokuwa wameisuka na jinsi watakavyotusambazia Watanzania “corona” ili tufikie hatua ya kufa kwa maelfu. Lakini wajinga hao hawakujua kwamba Tanzania ina Mungu aliye hai, mwenye nguvu zinazozidi nguvu ya fedha yao.
SIJUI k**a hata wewe Lema huko Bungeni uliamua kusisitizia kile alichobashiri Gates ama ulimwaga hisia zako tu, lakini hatimaye Aprili 2020 ilifika wala Watanzania hatukukumbwa na hayo mauaji ya kimbari kupitia COVID 19. Mungu alikuwa upande wetu, hatimaye vyuo na shule zetu zilifunguliwa, wanafunzi wakarudi madarasani, tukiwaacha hao waliokubali “lockdown” yao, sisi tukaendelea na mpango hadi tukafanikisha uchaguzi mkuu wetu.
Wakati wa kampeni ulipofika binafsi nikawategea wewe Godbless Lema uliyejivika joho la unabii na kututabiria Watanzania vifo vya halaiki, Freeman Mbowe aliyetuma mtandaoni hotuba ya kumtaka Magufuli atangaze kwamba Tanzania imeshindwa kupambana na “corona” ili tangazo kukiri kushindwa kuvutie misaada kutoka nje. Nilimsubiria Tundu Lissu ambaye kabla hajarejea nchini alizurula nchi kadhaa za Ulaya na Marekani akiisema vibaya serikali ya Tanzania. Niliwategea nisikie mnachowaambia wananchi kuhusu COVID 19, “lockdown” “curfew” “social distancing” na uvaaji “baracoa”
Niliuona kwenu unafiki ule ule wa Mafarisayo ambao Yesu aliwaambia “wanafiki ninyi wenye kuchuja mbu na kumeza ngamia” Tundu Lissu hadi anatoka nje ya uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere alivaa “baracoa” lakini alipoona jinsi washabiki walivyofurika wakimsubiri kwa hamu na wakiwa hawana “baracoa” alivua “baracoa” yake, akajumuika nao kwenye maandamano ambayo ninyi viongozi wa CHADEMA mlilazimisha.
Jiji la Dar es Salaam likatikiswa kwa maandamano ya CHADEMA yaliyochukua zaidi ya masaa manne, baadhi ya washabiki wenu walituma mtandaoni “post” za picha na video wakiita nyomi, wakati huo mliyasahau kabisa maelekezo ya WHO yanayotakiwa kutekelezwa katika kupambana na “corona.” Kwenye mikutano yenu hamkuhubiri chochote kuhusu “corona” badala yake mlisisitizia muujiza wa mtu kupigwa risasi 38 lakini hakufa.
Unafiki wenu uliipeleka “corona” likizo na kuyaweka kando kwa muda hayo maelekezo matatu ya WHO yaani “lockdown” uvaaji “baracoa” na “social distancing” unafiki wenu uliipeleka COVID 19 kwenye chumba cha mapumziko ilikuwa k**a “Half time” kwamba kampeni zitakapomalizika mkiwa washindi kwenye uchaguzi mkuu wa 2020 mkafanikiwa kushika dola, mngeendeleza maisha ya uhuru pasipo utisho wa “corona.” Lakini kwakuwa baada ya kampeni kumalizika hamkushinda ni k**a “corona” yenu nayo imemaliza likizo yake ama “Half time” imekwisha inabidi COVID 19 irudi tena uwanjani kuendelea na pambano kwenye kipindi chake cha pili.
Unafiki wenu unawafanya kurudia matangazo yenu ya awali mkidai kwamba sasa “corona” imerudi tena kwa kasi mpya na nguvu mpya, mlichokusudia ni kupandikiza hofu mioyoni mwa Watanzania na kusababisha taharuki ili umma “uki – panic” hatimaye serikali isalimu amri na kuikubali chanjo ili kufanikisha biashara za akina Gates. Siyo siri tajiri Bill Gates aliwekeza dola nyingi kwenye utafiti na utengenezwaji wa chanjo ya COVID 19.
Mmeyarudia pia mahubiri yenu ya awali, unafiki wenu umewasahaulisha kwamba kuna wakati mliwahi kuishi kwenye kipindi cha uhuru wa kutotawaliwa na COVID 19, mkaendesha kampeni mkiwa uhuru, hamkujali kwamba duniani kuna maelekezo ya “lockdown” “social distancing” na uvaaji “baracoa”
Godbless Lema unajinasibisha na wanaomtumikia Yesu lakini hukumbuki kisa cha wale wapelelezi 12 wakiwa Kardesh Bernea walivyotumwa na Musa wakaipeleleze nchi waliyoahidiwa? Waisraeli walibakiza mwendo wa siku 10 tu kuifikia nchi ya ahadi, lakini hawakuingia badala yake wakatanga tanga Jangwani miaka 40 kwasababu waliuamini uzushi wa wapelelezi 10. Mungu aliwakasirikia akasema “wana wenu na binti zenu watauchukua mzigo wa uasherati wenu.”
UASHERATI unaotajwa hapa siyo ule wa Gesti wala kwenye madanguro, bali ni uasherati wa moyoni, fikra za kitumwa, mawazo ya kitumwa na roho ya utumwa viliwafanya watumwa wale kuwahusudu wamisri k**a ninyi mnavyowahusudu wazungu hadi mnajitia upofu wa kutoona udhalimu wao, mnalilia mambo yasiyo na tija na yasiyowanufaisha Watanzania.
Lema “ume – post” ujumbe unaoonyesha Kilimanjaro wanakufa kwa “corona” lakini bado wanapelekewa mashindano ya marathoni, ukahukumu na kuuita upumbafu uliopitiliza! Hao wapumbafu unaowasema ni akina nani? JE, ni waliokufa kwa “corona” ama walio hai wanaokwenda Kilimanjaro? Hebu tutajie jina la mkimbiaji mmoja tu aliyekufa kwa “corona” ama aliyelazwa KCMC akiwa mahututi kwa COVID 19 aliyoipata Moshi?

WEWE Lema umekimbilia CANADA, huko siyo mbinguni pia “corona” kabla hujaingia Canada uliingia kwanza Kenya, ulijua Kenya ina “corona” hadi imekubali “lockdown!” Mmekazana kuilaumu serikali mkidai watu wengi wanakufa kwa “corona” ila serikali haitoi takwimu. SASA nakuorodheshea maelfu ya wanaouawa kimya kimya na “corona” wala vifo vyao havitangazwi, hata WHO haitaki vitangazwe.
(i) Naanza na “lockdown” WHO inajua na walimwengu wanajua kwamba nchi za Afrika hazina “Ambulance” zilizoko Ulaya. Berlin peke yake ina “Ambulance” nyingi kuliko zilizoko bara lote la Afrika zikijumlishwa Afrika kusini na Misri. Mji wa Ulaya ukitengwa, bado huduma kwa wajawazito hubaki hutolewa “Ambulance” huwafuata majumbani walikofungiwa na kuwafikisha Hospitali.
(ii) Raia wanaozidiwa ghafla kwa magonjwa mengine yasiyokuwa “corona” hufuatwa wakachukuliwa kwa “Ambulance” kutoka huko walikofungiwa hadi Hospitalini.
(iii) Wenye “appointment” za kuwaona madaktari kwenye tarehe zinazoangukia kipindi cha “lockdown” kwanza hujulikana mapema kutokana na mfumo wao wa Komputya, kisha hufuatwa na kupelekwa kuowana madakatari wao.
(iv) Lakini hebu niambie jiji la DSM lenye maeneo ya mabondeni yasiyofikiwa na gari k**a Kimara, Mwananyamala, Keko, Magomeni, Mkwajuni na mengineyo, Tanzania isiyokuwa na “Ambulance” za kuwafuata wagonjwa, wananchi wangapi watakufa watakapofungiwa ndani? Jibu unalo, hilo ndio linalothibitisha ninyi mnapigania mauaji ya halaiki, hampiganii haki ya mlalahoi kuishi.
(v) Eleza katika nchi za Afrika zilizoigiza “lockdown” nchi ipi ilitangaza ukweli kwamba katika siku 14 za kufungia watu wao ndani, kuna wajawazito kadhaa walijifungulia majumbani, kuna vichanga kadhaa vilikufa kwa kukosa huduma za wakunga, kuna wazazi kadhaa nao walikufa kwa kukosa huduma? Nani aliyetangaza kwamba waliougua malaria walikufa kiasi kadhaa katika kipindi cha “lockdown?” Nani aliyetangaza kwamba wenye ahadi za kuonana na madaktari walikufa walipokosa huduma? Nani aliye “post” video ya kumwonyesha mwananchi akihangaika na maiti chumbani mwake kwa siku 14 alizofungiwa ndani? JE, kuna Radio au Televisheni ya nchi yoyote iliwahi kuwapa raia nafasi ya kuelezea mikasa waliyoipata kwenye kipindi chote cha “lockdown?” Kwanini uhuru wa habari hizo unakandamizwa?
(vi) Godbless Lema habari hizo hufichwa ili zisiiabishe nchi iliyopokea maelekezo pasipo kuyatathmini, pia habari hufichwa ili zisiwaumbue WHO kwa kuwaonyesha kwamba wanatoa maelekezo yasiyotekelezeka, kwakuwa hayana uhalisia wowote kwenye maisha ya Waafrika ambao kiwango chao cha maendeleo hakifanani na Ulaya.

04/03/2021

MAGUFULI K**A NEBUKADNEZA MKUU WA DOLA YA BABELI
“BWANA ASIPOULINDA MJI YEYE AKASHEYE AFANAYA KAZI BURE”
Mwaka 2015 niliandika habari iliyochapishwa na Gazeti TAZAMA “Magufuli k**a Nebukadneza mkuu wa dola ya Babeli” nairudia tena baada ya kusoma Gazeti la RAIA MWEMA “sababu zilizowafanya mitume 11 wasimfuate Yesu majini” mwandishi amemshambulia sana Rais Magufuli.
Mwandishi anadai mwaka 2015 walipopiga kura kumchagua Rais, hawakutarajia Magufuli awe Askofu wa Tanzania, hawakufanya mabadiliko ili Magufuli awe Mwinjilisti mkazi wa Ikulu, Paroko wa kigango cha Magogoni. Hawakutarajia Magufuli awe Mhubiri mwenye upako uliopitiliza mwenye cheo cha unabii na utume wa Kiraisi! Mwinjilisti mfawidhi mwenye kupigiwa saluti.
Madai yote hayo kwasababu tu Rais Magufuli anasisitizia Watanzania kumtanguliza Mungu, hivi karibuni amewataka tena Watanzania kufunga kwa siku tatu ili kumsihi Mungu ainusuru Tanzania na “corona” ndipo mwandishi anapomwona Magufuli anajigeuza Askofu, Shehe, Mchungaji, Nabii na Mwinjilisti. Sijui mwandishi huyo anauchukuliaje uamuzi wa Kanisa Katoliki kumtangaza Nyerere mtakatifu wakati Nyerere hakuwahi kuwa Askofu wala kuwa Kardinali? Mwandishi amewanyamazia Watanzania wanaoihubiri “corona” kwa nguvu k**a kwamba “corona” ndio ugonjwa pekee unaoua!
Hao wote wanaopiga debe la “corona” siyo madaktari waliowatibu marehemu, siyo wasemaji wa familia za waliofiwa wala siyo wasemaji wa Taasisi ambazo marehemu walifanya nazo kazi, isipokuwa wapiga debe la “corona” wamejipa jukumu la kuikampenia “COVID 19 ” wanatumia umaarufu wa marehemu kuitangaza “corona” kibiashara, wanainadai imerudi kwa kasi mpya na nguvu mpya.
Wapiga debe la corona hawatofautiani na waliohamasisha mauaji ya kimbari nchini Rwanda mwaka 1994 waliotumia vyombo vya habari kuchochea mauaji, tofauti ni ndogo kwamba wahubiri wa “corona” wanahamasisha uuaji wa kisaikolojia na kiroho.
Mahubiri yao hasi yatawaacha Watanzania wengi wakiwa hai kimwili lakini ndani wakiwa wafu kiimani, walioaminishwa kwamba (i) “corona” iliyo duniani haishughulikiwi mbingunini
(ii) “corona” iliyotoka nje ya Afrika haisikii dawa yoyote iliyo ndani ya nchi
(iiii) “corona” haitibiki kwa njia za kiafrika isipokuwa tiba zitokazo nje.
(iv) Wapiga debe wanaamini ugonjwa uliotoka nje, unaomuua hata mzungu suluhisho lake haliwezi kupatikana Tanzania, wanaamini corona iliyotoka nje lazima suluhisho lake litoke nje.
Mahubiri yao yameambatana na lawama wanamlaumu Rais Magufuli kwasababu amekuwa jasiri! Wanatamani angesalimu amri awatangazie “superiors” wao walioko nje kwamba Tanzania nayo inakiri kwamba imeshindwa ili walitumie tangazo la kushindwa k**a sumaku ya kuvutia misaada.
Mwandishi anawasoma wapiga debe waliojiinua juu ya madaktari, waliowafunika wataalamu wa Afya na wanaoingilia hadi familia za marehemu wakijigeuza wasemaji wao. Mwandishi haioni jinai yao bali anaona dosari ya Magufuli hadi anamfananisha na Mtume Petro aliyethubutu kutembea juu ya bahari lakini mitume wengine 11 hawakumfuata.
Huyo ambaye leo tunamwita nabii zamani Waisraeli walimwita mwonaji, baadaye wakamwita anayesema kabla hayajatokea, wengine wakamwita mtabiri. Magufuli hasemi mambo kabla hayajatimia, mtu aliyetimiza sifa ya kusema mambo kabla hayajatokea na baadaye yakatokea ni Julius Nyerere, alisema mapema wataibuka watakaowatetea wanyonyaji bila aibu, hayo yametimia “Advocates” wa “imperialism” waliibukia Bungeni, wakaacha kumbukumbu za kudumu kwenye “Hansard” zinazoonyesha utetezi wao. SASA tusubiri kutimia alilosema Nyerere kwamba ataibuka Rais kwa ulevi atajitangaza Rais wa maisha.
Rais Magufuli siyo Askofu, siyo Mwinjilisti, siyo Shehe, siyo mchungaji, siyo Paroko wala siyo Nabii bali ni zaidi ya Nabii, zaidi ya Askofu, Shehe, Mwinjilisti, Paroko na zaidi ya Mchungaji. Kwasababu ameinuliwa na Mungu kwa wakati wake ili afanye wasiyofanya Maaskofu na Mashehe na Wachungaji na Wainjilisti, Magufuli anamtumikia Mungu kwenye nafasi yake ya Urais.
Neno la Mungu linasema msh*taki wa wenye haki Ibilisi ni k**a Simba angurumaye akitafuta mtu ammeze, Shetani amefananishwa na simba aliyezeeka asiyeweza kumrukia mnyama uso kwa uso, bali hujificha mahali akaunguruma kuwatisha wanyama watakaokimbia sauti yake wakakutane na simba wanaok**ata.
David Camerun aliyekuwa Waziri mkuu wa Uingereza aliunguruma kwenye Jumuia ya madola akizitaka nchi za Afrika zibadilishe katiba zao ili zitambue ndoa za jinsia moja, Rais wa Marekani Barack Obama na Cameruni , walitishia kwamba nchi isiyobadilisha katiba yaani isiyoukubali ushoga, isitarajie kupokea msaada wowote kutoka Jumuia ya Ulaya wala Marekani. Tanzania kwakuwa ilitaka kuendelea kupata fedha za bure ilitikiswa, ikaanzisha mchakato wa katiba mpya.
Hao wababe walipounguruma kwa niaba ya Ibilisi hakuna Askofu, Mchungaji, Shehe, Nabii, Mtume wala Mwinjilisti aliyesimama na kweli ya Mungu kuwaambia hapana! Ni Robert Mugabe tu Rais wa Zimbabwe aliyekuwa jasiri kumwambia Obama “ukija Zimbabwe kuhamasisha ushoga itabidi kwanza mimi nikuoe ili tuonyeshe mfano.”
Lakini wengine wote hata wanaojiita wainjilisti wakubwa wa kimataifa, hakuna aliyethubutu kuupinga ufisadi huo ili kuinusuru Afrika. Pope alinyamaza kimya hakuthubutu kuwapigania wakatoliki walioko Afrika, ikumbukwe Yesu alisema “atakaporudi tena mwana wa Adamu, ataikuta imani duniani?” Yesu alimaanisha ataikuta imani ile ile aliyoasisi? Papa hadi leo kwenye suala la ushoga anajigongagonga hayuko uwazi kukiri k**a alivyofundisha Yesu kwamba “ndiyo yenu iwe ndiyo na siyo yenu iwe siyo” lolote lisiloangukia kwenye ndiyo wala hapana linatoka kwa yule MwoVU.
Kwanini namfananisha magufuli na nebukadneza? Kwasababu Mwenyezi Mungu huwainua watu ili kutimiza makusudi yake. Ikiwa amemuinua Magufuli kuwafikishia ujumbe walimwengu, Waafrika na Watanzania, hakuna mwenye ubavu wa kuzuia wala kumwambia Mungu huyo ni Rais wetu, tulimchagua wenyewe kwa kura zetu, hawezi kutumika k**a chombo chako Mungu wakati Mashehe na Maaskofu wapo!
Mungu aliwahi kumtumia Punda kusema k**a mwanadamu, kwasababu Nabii Baalamu alipata wazimu alipolipwa kiasi kikubwa cha fedha ili afanye waliyotaka wanadamu kuacha aliyoyataka Mungu. Hata leo dini “zikibiasharaishwa” (commercialized) viongozi wake wanapagawishwa na nguvu ya fedha hadi wanapoteza mamlaka ya kiroho “moral authority.”
Mfano hai Askofu mkuu wa dhehebu la Anglican alijitangaza kuwa shoga, hakuna Mchungaji wala muumini wa Afrika aliyethubutu kujitenga na Anglikani ya Ulaya wala Marekani, kuashiria kuuchukia uchafu huo! Hakuna mwenye jeuri ya kujitenga azikose dola za Marekani na Euro za Ulaya! Hawa ndio watakaofungisha ndoa za jinsia moja kwenye madhehebu yao, ni mtihani mgumu kati ya kuikiri nguvu ya Yesu kwa kushik**ana naye ama kuikiri nguvu ya fedha na kumkana Yesu. Fedha ndio ilimfanya Nabii Baalamu apate wazimu hadi akasababisha Punda kusema k**a binaadamu.
Mwenyezi Mungu hafungwi na mifumo ya dini na madhehebu, wala kwenye mapambano ya ukombozi Mungu hawekewi mipaka na wanadamu. Wapigania uhuru walioongoza TANU walimhusisha Mungu kwenye mapambano yao, mashehe walimshurutisha Julius Nyerere kufunga pamoja nao ingawaje walimfahamu hakuwa mwislamu.
Wakati wa mapambano Nyerere aliwahi kuulizwa swali ingekuwaje endapo Mwingereza angegoma kutoa uhuru? Waliomuuliza walitarajia Nyerere ajibu k**a kiongozi mwoga ama ajibu kishujaa ili nao Watanganyika wachukue msimamo k**a wa Kenya ambako Mzee Jommo Kenyata alikuwa amewaingiza wananchi kwenye mapambano ya umwagaji damu, waliyaita MAUMAU yaani Mzungu Arudi Ulaya Mwafrika Apate Uhuru.
Nyerere alijibu kwa utulivu kwamba Gavana akigoma kutoka, tutamsh*takia Malkia, asipotusikiliza Malkia tutash*taki Umoja wa Mataifa, huo usipotusikiliza tutamsh*takia Mungu. Huo ni uthibitisho kwamb a tangu awali Watanganyika walimtanguliza Mungu, walimwamini na kumkiri kwa kila gumu walilokutana nalo maishani mwao, ndio maana uhuru ulipopatikana waasisi walikumbuka kumtaja Mungu na kumkiri kwenye wimbo wetu wa Taifa.
Tunapoimba “Mungu ibariki Afrika, uwabariki viongozi wake, uwape hekima, kwakuwa hekima na umoja ndio ngao zetu ama kinga yetu sisi Afrika na watu wake” dua hili halielekezwi kwa Jabali wala sanamu la kuchongwa lisilosikia, lisilojibu wala lisiloweza kufanya lolote, bali tunamwomba Mungu aliye hai.
Watanzania tunapoimba “Mungu ibariki Tanzania, dumisha uhuru na umoja kwa wote, wanawake, wanaume na watoto” hatuombi kwa HAKUNA, isiyoyosikia, isiyoitika wala isiyotenda. Tunamwomba yeye ambaye yuko, mwaminifu na wa haki, hao waliotetereka kiimani yaani wanaoamini kwamba maendeleo ya sayansi na tekinolojia yatakuwa mbadala wa Mungu wasitulazimishe kuikubali hiyo imani yao iliyokengeuka, imani iliyompindua Mungu duniani, ikamgeuza awe Mungu wa mbinguni tu.
SISI wengine bado tunaamini
(i) Mungu anatakiwa kutawala dunia 100%.
(ii) Mungu k**a alivyo Mungu huko Mbinguni ndivyo alivyo Mungu hapa duniani
(iii) Mungu k**a anavyohusika na mbinguni ndivyo anavyohusika pia na dunia yetu kwa kiasi kile kile anachohusika mbinguni.
(iv) Mungu ni yule yule wa zamani wa sasa na baadaye
Mtu anayejiona amesoma, ameelimika, ameendelea na amepiga hatua kisayansi na kitekinolojia na kwahiyo awe amepevuka kiasi kwamba upevu wake unamtosha, unamfanya asimtegemee tena Mungu maishani mwake, huyo tumwambie wazi uasi wake asiuingiza kwenye dola. KWASABABU dola ni yetu wote tunaoamini na wasioamini, Rais Magufuli ni wetu wote, wasitokee wanaolazimisha Rais wa Tanzania awe mali ya wasioamini tu.
Tanzania ni dola iliyoanza na Mungu tangu ikiitwa Tanganyika, imeendelea na Mungu hadi leo na itaendelea na Mungu hadi kiama, wanaweza kuibuka viongozi wakengeufu lakini bado hatakosekana Mtanzania japo mmoja wa kusimama kwa niaba ya Mungu.
Mwenyezi Mungu kwa kinywa cha Nabii Yeremia anamwita Nebukadneza mtumishi wangu, Nabii Yeremia amelirudia neno hilo “mtumishi wangu Nebukadneza” mara sita. Wakati Nabii Yeremia akimtaja Nebukadneza Mfalme wa Babeli k**a mtumishi wa Mungu, huyo Nebukadneza mwenyewe hakuwa akimjua Mungu wa Waisraeli. Nebukadneza alikuwa na miungu yake ya kibabeli. Kumbe ilikuwaje Mungu asimwite mtumishi wangu Mfalme Sedekia wa dola ya kidini ya Israeli, bali amwite Nebukadneza ambaye kulingana na dini ya wayahudi aliitwa “kafiri?”
Kwanini Mungu hakuwaita Makuhani na viongozi wa dini ya kiyahudi watumishi wake bali akamwita Nebuukadneza ambaye leo kwa viwango vya madhehebu yaliyotoka Ulaya ni “pagano” ama “gentile?” Hapa ndipo unatakiwa uelewa kwamba Mungu hafugwi kwenye taratibu za wanadamu, Nebukadneza aliitwa mtumishi wa Mungu kwasababu aliitwa kulitumikia shauri la Mungu.
Nebukadneza aliitwa mtumishi wa Mungu kwasababu kwa nafasi yake k**a Mfalme aliutimiza mpango wa Mungu, inabidi tukubali kwamba kuna mambo hapa duniani ambayo Mungu hawezi kuwatuma Malaika kuyafanya ili malengo (mapenzi) yake yatimizwe, bali atawatumia wanadamu kwa nafasi zao ama kwa kaliba zao.

03/03/2021

MAGUFULI K**A NEBUKADNEZA MKUU WA DOLA YA BABELI
“BWANA ASIPOULINDA MJI YEYE AKASHEYE AFANAYA KAZI BURE”
Mwaka 2015 niliandika habari iliyochapishwa na Gazeti la TAZAMA “Magufuli k**a Nebukadneza mkuu wa dola ya Babeli” nairudia tena baada ya kusoma Gazeti la RAIA MWEMA, mwandishi anayejiita MWANA KIJIJI ameandika “sababu zilizowafanya mitume 11 wasimfuate Yesu majini” amemshambulia sana Rais Magufuli.
Mwandishi anadai mwaka 2015 walipopiga kura kumchagua Rais, hawakutarajia Magufuli awe Askofu wa Tanzania, hawakufanya mabadiliko ili Magufuli awe Mwinjilisti mkazi wa Ikulu, Paroko wa kigango cha Magogoni. Hawakutarajia Magufuli awe Mhubiri mwenye upako uliopitiliza mwenye cheo cha unabii na utume wa Kiraisi! Mwinjilisti mfawidhi mwenye kupigiwa saluti.
KWASABABU Rais anasisitizia Watanzania kumtanguliza Mungu, ndipo mwandishi anaona Magufuli amejigeuza Askofu, Shehe, Mchungaji, Nabii na Mwinjilisti, hivi karibuni amewataka Watanzania kufunga tena kwa siku tatu ili kumsihi Mungu ainusuru nchi na COVID 19.
Sijui mwandishi huyo anaichukuliaje hatua ya kumtangaza Nyerere k**a mtakatifu wa kanisa katoliki kutoka Afrika wakati Nyerere hakuwahi kuwa Askofu? Lakini mwandishi amewaachia Watanzania wanaoihubiri “corona” k**a kwamba hata Adamu na Hawa walikufa kwa COVID 19 .
Wapiga debe la corona wote siyo madaktari waliowatibu marehemu, siyo wasemaji wa familia za wafiwa wala siyo wasemaji wa Taasisi ambazo marehemu walifanya nazo kazi, lakini wamejipa majukumu ya kuiinua corona wakiutumia umaarufu wa marehemu k**a tangazo la kibiashara, kuinadai COVID 19 wakisema imerudi kwa kasi mpya na nguvu mpya.
Wapiga debe la corona hawatofautiani na waliohamasisha mauaji ya kimbari nchini Rwanda mwaka 1994 waliotumia vyombo vya habari kuchochea mauaji, tofauti ni ndogo kwamba wahubiri wa corona wanahamasisha uuaji wa kisaikolojia na kiroho.
Mahubiri yao hasi yatawaacha Watanzania wengi wakiwa hai kimwili lakini ndani wakiwa wafu kiimani, walioaminishwa kwamba corona iliyo duniani haishughulikiwi mbingunini, corona iliyotoka nje ya Afrika haisikii dawa yoyote iliyo ndani ya nchi, corona haitibiki kwa njia za kiafrika isipokuwa tiba zitokazo nje. Wanaoamini ugonjwa uliotoka nje, unaomuua hata mzungu suluhisho lake haliwezi kupatikana Tanzania, wanaamini corona iliyotoka nje suluhisho lake liko nje.
Mahubiri yao yameambatana na lawama kumlaumu Rais Magufuli kwasababu amekuwa jasiri! Wanatamani angesalimu amri awatangazia “superiors” wao walioko nje kwamba Tanzania nayo inakiri kushindwa ili waitumie hali ya kushindwa k**a sumaku ya kuvutia misaada.
Mwandishi anawasoma wapiga debe waliojiinua juu ya madaktari, waliowafunika wataalamu wa Afya na wanaoingilia hata familia za marehemu wakijigeuza wasemaji wao. Mwandishi haioni jinai yao bali anaona tu dosari ya Magufuli hadi anamfananisha na Mtume Petro aliyethubutu kutembea juu ya bahari lakini mitume wengine 11 hawakumfuata.
MAGUFULI NI ZAIDI YA NABII
Leo tunayemwita nabii zamani Waisraeli walimwita mwonaji, baadaye wakamwita mwenye kusema kabla hayajatokea, wengine wakasema anatabiri. Magufuli hasemi mambo kabla hayajatimia, mtu anayetimiza sifa ya kusema mambo kabla hayajatokea na baadaye yakatokea ni Julius Nyerere, alisema kabla wataibuka watetezi wa wanyonyaji, hayo yametimia “Advocates” wa “imperialism” waliibukia Bungeni, wakaacha kumbukumbu ya kudumu kwenye “Hansard” kuhusu utetezi wao. SASA tusubiri kutimia alilosema Nyerere kwamba ataibuka Rais ambaye kwa ulevi atajitangaza Rais wa maisha.
Rais Magufuli siyo Askofu, siyo Mwinjilisti, siyo Shehe, siyo mchungaji, siyo Paroko wala siyo Nabii bali ni zaidi ya Askofu, zaidi ya Shehe, zaidi ya Mwinjilisti, zaidi ya Paroko, zaidi ya Mchungaji na zaidi ya Nabii. Kwasababu ameinuliwa na Mungu kwa wakati wake ili afanye wasiyoyaweza Maaskofu na Mashehe na Wachungaji na Wainjilisti, Magufuli anamtumikia Mungu kwa nafasi yake ya Urais.
Neno la Mungu linasema msh*taki wa wenye haki Ibilisi ni k**a Simba angurumaye akitafuta mtu ili ammeze. Shetani k**a simba aliyezeeka asiyeweza kumrukia mnyama, hujificha mahali akaunguruma ili wanyama watakaokimbia sauti yake wakutane na simba wak**ataji.
David Camerun aliyekuwa Waziri mkuu wa Uingereza aliunguruma kwenye Jumuia ya madola akizitaka nchi za Afrika zibadilishe katiba zao kutambua ndoa za jinsia moja, Barack Obama wa US na Cameruni wa UK walisema wazi nchi isiyobadilisha katiba (isiyoukubali ushoga) isitarajie haitapokea msaada wowote kutoka Jumuia ya Ulaya wala Marekani. Tanzania kwasababu iliyotaka fedha za bure ilitikiswa, ikaanzisha mchakato wa katiba mpya.
Hao wababe walipounguruma kwa niaba ya Ibilisi hakuna Askofu, Mchungaji, Shehe, Nabii, Mtume wala Mwinjilisti aliyesimama upande wa Mungu kuwaambia hapana! Ni Robert Mugabe tu Rais wa Zimbabwe aliyekuwa jasiri kumwambia Obama “ukija Zimbabwe kuhamasisha ushoga itabidi kwanza mimi nikuoe wewe Obama ili tuonyeshe mfano.”
Lakini wengine wote hata hao wanaotamba k**a wainjilisti wa kimataifa, hakuna yeyote aliyethubutu kuugusa (kuupinga) ufisadi huo ili kuinusuru Afrika. Hata Pope alinyamaza kimya hakuthubutu kuwapigania wakatoliki walioko Afrika, ikumbukwe Yesu alisema “atakaporudi tena mwana wa Adamu, ataikuta imani duniani?” Yesu alimaanisha ataikuta imani ile ile aliyoasisi? Papa hadi leo kwenye suala la ushoga anajigongagonga hayuko uwazi kukiri k**a alivyofundisha Yesu kwamba “ndiyo yenu iwe ndiyo na siyo yenu iwe siyo” lolote lisiloangukia kwenye ndiyo wala hapana linatoka kwa yule Mwovu.
KWANINI NAMFANANISHA MAGUFULI NA NEBUKADNEZA?
KWASABABU Mwenyezi Mungu huwainua watu ili kutimiza makusudi yake ikiwa amemuinua Magufuli kuwafikishia ujumbe Walimwengu, Waafrika na Watanzania, hakuna mwenye ubavu kuzuia wala atakayemwambia Mungu huyo ni Rais wetu tuliyemchagua wenyewe kwa kura zetu, hawezi kutumika k**a chombo chako wakati Mashehe na Maaskofu wapo!
Mungu alimtumia Punda akasema k**a mwanadamu, baada ya Nabii Baalamu kutiwa wazimu na kiasi kikubwa cha fedha alichofungashiwa ili afanye waliyotaka wanadamu hakujali aliyoyataka Mungu. Hata leo dini “zikibiasharaishwa” (commercialized) wenye dini watapagawishwa na nguvu ya fedha, hadi kupoteza mamlaka ya kiroho “moral authority” mfano hai Askofu mkuu wa dhehebu la Anglican alijitangaza kuwa shoga, hakuna Mchungaji wala muumini wa Afrika aliyethubutu kujitenga na Anglikani ya Ulaya wala Marekani kuashiria kuuchukia uchafu huo! Hakuna mwenye jeuri ya kujitenga azikose dola za Marekani na Euro za Ulaya! Hawa ndio watakaofungisha ndoa za jinsia moja kwenye madhehebu yao, ni mtihani mgumu kati ya kuikiri nguvu ya Yesu kwa kushik**ana naye ama kuikiri nguvu ya fedha na kumkana, ndio yaliyomshinda Nabii Baalamu hadi wazimu wake ukasababisha Punda aseme k**a binaadamu.
Mwenyezi Mungu hafungwi na mifumo ya madhehebu ya dini, wala kwenye mapambano ya ukombozi Mungu hawekewa mipaka na wanadamu. Walioongoza TANU walimhusisha Mungu katika mapambano yao walipopigania uhuru, mashehe walimshurutisha Julius Nyerere kufunga pamoja nao licha ya kumfahamu hakuwa mwislamu.
Wakati huo wa mapambano Nyerere aliulizwa swali itakuwaje endapo Mwingereza atagoma kutoa uhuru? Waliomuuliza swali hilo walimtegea Nyerere aidha kujibu k**a kiongozi mwoga ama kujibu kishujaa kwamba na Watanganyika nao watachukua msimamo wa Kenya. Mzee Jommo Kenyata alikuwa ameiingiza Kenya kwenye mapambano ya umwagaji damu waliyaita MAUMAU yaani Mzungu Arudi Ulaya Mwafrika Apate Uhuru.
Nyerere alijibu kwa utulivu kwamba Gavana akigoma kutoka, tutamsh*takia Malkia, asipotusikiliza Malkia tutash*taki Umoja wa Mataifa, huo usipotusikiliza tutamsh*takia Mungu. Huo ni uthibitisho kwamb a tangu awali Watanganyika walimtanguliza Mungu walimwamini na kumkiri kwa kila gumu walilokutana nalo maishani, ndio maana baada ya uhuru kupatikana waasisi walikumbuka kumtaja Mungu (kumkiri) kwenye wimbo wetu wa Taifa.
Tunapoimba “Mungu ibariki Afrika, uwabariki viongozi wake, uwape hekima, kwakuwa hekima na umoja ndio ngao zetu ama kinga yetu sisi Afrika na watu wake” dua hili halielekezwi kwa Jabali wala sanamu la kufikirika lisilosikia, lisilojibu wala lisiloweza kufanya lolote, bali tunamwomba Mungu aliye hai.
Watanzania tunapoimba “Mungu ibariki Tanzania, dumisha uhuru na umoja kwa wote, wanawake, wanaume na watoto” hatuombi kwa HAKUNA, isiyoyosikia, isiyoitika wala isiyotenda. Tunamwomba yeye ambaye yuko, mwaminifu na wa haki, hao waliotetereka kiimani yaani wanaoamini kwamba maendeleo ya sayansi na tekinolojia yatakuwa mbadala wa Mungu wasitulazimishe kuikubali hiyo imani yao iliyompindua Mungu duniani, ikamgeuza aishie kuwa Mungu wa mbinguni tu, bado Mungu anatakiwa kutawala dunia 100%.
(i) Mungu k**a alivyo Mungu huko Mbinguni ndivyo alivyo Mungu hapa duniani
(ii) Mungu k**a anavyohusika Mbinguni anahusika pia na dunia yetu kwa kiasi kile kile anachohusika mbinguni.
(iii) Mungu ni yule yule wa zamani wa sasa na baadaye
Mtu anayeona binaadamu wa leo amesoma, ameelimika, ameendelea na kupiga hatua kubwa kisayansi na kitekinolojia na kwahiyo awe amepevuka kiasi kwamba upevu wake unatosha kumfanya asimtegemee tena Mungu maishani mwake, huyo tumwambie wazi uasi wake asiuingiza kwenye dola, kwasababu dola ni yetu wote tunaoamini na wasioamini. Rais wa nchi ni wetu wote, wasitokee wengine kulazimisha kwamba Rais wa Tanzania awe mali ya wasioamini tu.
Tanzania ni dola iliyoanza na Mungu tangu ikiitwa Tanganyika, imeendelea na Mungu hadi leo na itaendelea na Mungu hadi kiama, wanaweza kuibuka viongozi wakengeufu lakini bado hatakosekana japo Mtanzania mmoja mwenye kumcha Mungu.
NABII WA YEREMIA NA MFALME NEBUKADNEZA
Mwenyezi Mungu kwa kinywa cha Nabii Yeremia anamwita Nebukadneza mtumishi wangu, Nabii Yeremia amelirudia neno hilo “mtumishi wangu Nebukadneza” mara sita. Wakati Yeremia akimtaja Nebukadneza k**a mtumishi wa Mungu, huyo Nebukadneza mwenyewe hakuwa akimjua Mungu wa Waisraeli. Nebukadneza alikuwa na miungu yake ya kibabeli, swali ilikuwaje Mungu asimwite mtumishi wangu Mfalme Sedekia wa dola ya kidini ya Israeli, badala yake amwite Nebukadneza ambaye mbele ya dini ya wayahudi alikuwa “kafiri?”
Ilikuwaje Mungu asiwaite Makuhani na viongozi wa dini ya kiyahudi watumishi wake bali amwite Nebuukadneza ambaye leo kwa viwango vya madhehebu yaliyotoka Ulaya ni “pagano” ama “gentiles?” Hapa ndipo unatakiwa uelewa kwamba Mungu hafugwi kwenye taratibu za wanadamu, Nebukadneza aliitwa mtumishi wa Mungu kwasababu aliitwa kulitumikia shauri la Mungu.
Nebukadneza aliitwa mtumishi wa Mungu kwasababu kwa nafasi yake k**a Mfalme aliutimiza mpango wa Mungu, inabidi tukubali kwamba kuna mambo hapa duniani ambayo Mungu hawezi kuwatuma Malaika kuyafanya ili malengo (mapenzi) yake yatimizwe, bali atawatumia wanadamu kwa nafasi zao ama kaliba zao.

Address

MAGOMENI
Dar Es Salam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jjifunze ZaidiI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category