12/11/2023
“Basi, Mwenyezi-Mungu akamwambia Abramu, “ONDOKA katika nchi yako, ACHA JAMAA YAKO na nyumba ya baba yako, uende katika nchi nitakayokuonesha.
Nitakufanya WEWE kuwa taifa KUBWA, nitakubariki na kulikuza JINA LAKO, nawe UWE BARAKA.”
Mwanzo 12:1-2 BHN
Moja ya MCHAKATO muhimu wa kuelekea kwenye UKUU wako ni “Intentional Separation”.
Yaani, KUAMUA na KUKUBALI kuwa mbali na WATU, hasa ULIOWAZOEA.
Mungu alipotaka kumfanya Abraham kuwa MKUU na KUKUZA JINA LAKE, maagizo ya kwanza yalikuwa ni kutoka katika JAMII aliyoizoea, kwenda mbali na NDUGU na JAMAA zake.
Kuondoka inaweza kumaanisha: “Mental Separation”- Kuanza kuwaza tofauti na ndugu na jamaa zako wanavyowaza.
“Behavioural Separation” inayohusisha kuwa na tabia tofauti kabisa na walizonazo ndugu/jamaa zako au;
“Physical Separation” ambayo inahusisha kuondoka na kukaa mahali ambapo ni mbali na eneo ambalo ndugu/jamaa zako wapo.
Aina yoyote katika hizi, itakuwa na GHARAMA kubwa sana kwenye maisha yako, ila lazima uwe na UJASIRI wa kuifanya.
NAKUTAKIA JUMAPILI NJEMA.
https://chat.whatsapp.com/B9ci0VJUVVJLeVNhC8DbyW 0692432722